21.7.14

TAMBUA KUSUDI LA NDOA NA NAFASI YA MWANAMKE KATIKA NDOA


TAMBUA KUSUDI LA  NDOA NA NAFASI YA MWANAMKE KATIKA NDOA
I) Ndoa kama taasisi ya Mungu.
Kwa kijana anayejitambua mara nyingi unapofikia wakati kama huu wa kutafuta mwenzi, kwake huwa ni kipindi ambacho ni kugumu sana, kwa sababu anajua anakokwenda hivyo mke kama ndiye msaidizi lazima uumize akili, lakini kwa yule asiyejitambua, huwa anaona bora kuoa yeyote yule ilimradi kampenda kwa mwonekano wake na ndiyo hizo ndoa ambazo hazidumu sana.
       Kosea nguo kuvaa, watakwelekeza ubadilishe, kosea njia watakwelekeza na utarudi, kosea kununua kiatu pengine unaweza ukabadilisha au ukauza na kununua kingine, lakini ukikosea kuoa/kuolewa, kwakweli utakuwa umeharibu dira yako na kusudi la Mungu ndani yako. Ndoa siyo kitu rahisi rahisi tu, kwa kipindi kifupi hiki ninapokuwa kwenye huduma sehemu mbalimbali hapa Tanzania huwa tunakutana na matatizo ya ndoa, hasa kwa ndoa za Kikristo ukifunga umefunga, nimejifunza vitu vingi sana mpaka nikaingia kwenye maombi nipate kujua kwanini Mungu amemua kutokutengana pindi ndoa zinaposumbua? Kwanini mara nyingi ndoa zinasumbua?

i)                    Elewa kusudi la ndoa kama kijana
a)      Ndoa yawakilisha umoja kati ya washiriki watatu wa utatu Mtakatifu (Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu). Kama vile washiriki watatu wa Utatu Mtakatifu walivyo nafsi tofauti bali Mungu mmoja, ndivyo Mume na mke ni tofauti bali wameunganishwa na kuwa mwili mmoja (Mwz 2:24).
b)      Ndoa ni mfano wa uhusiano wa Yesu na Kanisa lake (Efe 5:22-33)
a.       Mke na amtii mumewe kama kanisa linavyomtii Kristo.
b.      Mume na ampende mkewe kama Kristo alivyolipenda kanisa akajitoa kwa ajili ya kanisa.
c.       Inamana wanandoa wanapaswa kuwa mfano wa uhusiano wa Kriso na kanisa lake.

c)      Kutokana na kitabu cha Mwanzo na vitabu vingine utaona makusudi ya ndoa yalivyojitokeza.
a.      Urafiki, “BWANA Mungu akasema, si vema huyo mtu awe peke   yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye” (Mwz 2:18)
b.      Umoja, “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja” (Mwz 2:24), Kunatofauti kati ya Umoja na kuwa pamoja, umoja ina maana nia moja, lengo moja, mawazo yasiyopingana n.k. ndoa nyingi wanakuwa pamoja lakini hawana umoja, ni sawa na kwenye mkusanyiko kama msibani au harusini, kwa wale wanakuwa pamoja lakini utashangaa hawana umoja, huyu akiambiwa hivi yeye anafanya vile, mwingine anawaza ataondoka saa fulani kwenda kwake.
c.       Uzao, ‘….Mungu akawambia Zaeni mkaongezeke, mkaijaze nchi na kuitiisha;….”  (Mwz 1:28)
“Mungu akambariki Nuhu na wanawe, akawaambia, Zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi” (Mwz 9:1).
d.      Starehe, “Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala” (Mwz 3:16),
“Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye siku zote za maisha yako….” (Mhubiri 9:9)
e.       Ulinzi dhidi ya uasherati, “Lakini ikiwa hawawezi kujizuia na waoe; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa” (1Kor 7:9)

    II) Nafasi ya Mwanamke kwenye ndoa
             Mwanamke kwenye ndoa katambulishwa kama msaidizi wa mwanamume hivyo inamaana kwamba mwanamume hawezi kujitosheleza yeye kama yeye ni mpaka kuwepo mwanamke kama msaidizi wake, na anaposema “Msaidizi wa kufanana” inamaansha “wa kukubaliana, “Mwenzi” wa mwanamume, mwenyekumkamilisha na kumsaidia, siyo kuwa mtumwa wake. Na hii inamaanisha:
i)                    Mwanaume anahitaji masaada ili kuijaza nchi na jukumu la kuitiisha nchi.
ii)                  “Msaidizi” ni cheo kikubwa na cha heshima sana.
a)      Mungu mwenyewe wakati mwingine huitwa “Msaidizi”,
“ Ee BWANA, usikie, unirehemu, BWANA, uwe msaidizi wangu”, (Zaburi 30:10),
 “……Bwana atanitunza, Ndiwe msaidizi wangu na mwokozi wangu….” (Zaburi 40:17), “
 “Hata twathubutu kusema Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?” (Ebr 13:6),
Ukitafakari vizuri katika mistari hiyo utatambua neno msaidi limetumika kumpa nafasi Mungu anayojitokeza kwa ajili ya mwanadamu, hivyo ni kama Mwanadamu hawezi kufanya jambo bila huyu msaidizi Mungu.
b)      Roho Mtakatifu katumika kama “Msaidizi” wetu,
“Nami nimemwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele, ndiye Roho wa kweli…” (Yoh 14:16,17),
“Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia” (Yoh 14:26),
Bwana Yesu Asifiwe! Endelea kusoma na (Yoh 15:26; 16:7) .

Sasa kama hiki cheo cha “Msaidizi ni chakumstahili muumba wa ulimwengu, basi inamaana hata mwanamke anahadhi kubwa ya yeye kuwa “Msaidizi” wa mwanamume na hivyo mke inabidi ajivunie kwa kuwa nacho hicho cheo, na kama ulikuwa hujui wewe mwanaume kwa kumdharau mke wako nakushauri umpigie na magoti ukamwombe msamaha endapo ulikuwa unamdharau.
                                Itanendelea ............................................... 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni