- TAFUTA MAHALI PAZURI PENYE UTULIVU. (Marko 1:35)
Ili uweze kuomba kwa utulivu na kwa umakini, chagua au
tafuta mahali pazuri patakapokupa utulivu katika kuomba (Concentration in
prayer). Ndio maana Mungu alipenda kuongea na Musa mlimani, (Kutoka 24:12-18).
Hata Yesu alizoea kwenda kuombea mlimani, mahali palipo mbali na vurugu za
watu, alipenda kwenda mlimani, (Mathayo 14:22-23). Tafuta mahali patulivu;
chumbani, kanisani, mlimani, n.k (Mt 6:5-6).
Mazingira yakiwa na kelele, htaweza kuomba kwa umakini, na hata usikivu wa kumwelewa Mungu hata akisema nawe huwa inakuwa ni ngumu sana.
- TENGA MUDA MZURI (Mhubiri 3:1-7)
Ukitaka uombe kwa umakini mzuri na kwa mzigo, chagua muda
mzuri ambao utakuwa unahakikisha akili yako na mwili wako viko freshi. Usije
ukalazimisha kuomba hata kama akili yako au mwili wako umechoka sana. Kila
jambo lina wakati wake. Kama umechoka sana, huo si muda wa kuomba, bali ni wa
kupumzika. Usilazimishe ratiba. Ni bora upumzike ili baadaye uweze kuomba
vizuri. Usije ukajikuta unapiga tu miayo na hujui unaomba nini. Penda kuomba
wakati unanguvu ya akili a mwili, ili uwe makini kuongea na Mungu kwa akili
timamu. Ndio maana Yesu alipenda kuamka alfajiri sana kwenda kuomba mlimani.
Hata
nyumbani, jaribu kutenga muda wa kuangalia TV, na siyo muda wote unatazama TV
mpaka inakuondolea mawazo ya kuomba. Mimi huwa nina muda maalumu wa kutazama,
ni tarifa ya habari saa 2 usiku mpaka saa 3:30 ndipo ninazima, na ninaenelea na
ratiba zingine. Nidhamu ya kumtafuta Mungu kwa kumtengea muda wa kuongea naye
ni vizuri zaidi kwani itakutengenezea heshima mbele zake. Biblia inasema
”nawapanda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii watanina” Mith 8:17.
ukimheshimu Mungu kwa kutenga muda kwa ajili yake, na yeye atakuheshimu.
- OMBA KATIKA ROHO (Nena kwa Lugha). (Rum:26-27, Waefeso 6:18)
Kuomba kwa Roho, yaani kunena kwa Lugha, kunamfanya Roho
Mtakatifu anayejua kuchunguza mioyo yetu na haja tulizonazo, anakamata ulimi
wako kuhakikisha anakuombea vile Mungu atakavyo, na kwa kutegemeana na mzigo
ulionao mpaka uishe ndani yako ndipo anakuachia. Hivyo kwasababu mahitaji
tunayomengi, huwa unaweza ukajikuta unaomba kwa muda mrefu zaidi mpaka Mungu
aone mpenyo wa kuachilia ukiombacho. Tunapoomba kwa akili za kibinadamu, mungu
anasikia pia, lakini maombi yako yanakuwa na mipaka, kwa sababu akili yta mtu
haijui kila kitu. Bali Roho wa Mungu anajua kila kitu. Naye hutupa kipawa cha
kuomba kwa lugha ya mbinguni iliyo bora zaidi. (Yuda 1:20, Marko 16:17, 1Kor
14:1-4, 15-16,7)
- WAKATI MWINGINE OMBA KWA KUFUNGA (Mathayo 6:16-18)
Kufunga kunasaidia kudhoofisha mwili, ili roho iwe makini
zaidi kuongea na Mungu kwa kina zaidi. Mwili huu siku zote haupendi kufanya
mambo ya Mungu. Unapofunga, unajionesha mbele za Mungu kujitoa kwako kama
dhabihu iliyo hai. Unampa Mungu kipau mbele kuliko vyote, ni badala ya kutoa
sadaka ya pesa au ya aina yoyote, kwani kule kuomba tu ni sadaka tosha mbele za
Mungu (Mith 15:8). Kama Yesu alivyojitoa kuwa dhabihu takatifu kwa Mungu kwa
ajili ya mwanadamu, ndivyo vivyo hivyo, unapofunga unajitolea kwa ajili yako na
kwa niaba ya wengine, (Isaya 58).
Mara
nyingine, kama unapenda kufanya ibada jioni, pengine majira ya saa 2 usiku, kwa
watu wengi muda huo unakuwa ni muda wa chakula cha jioni. Lakini nataka
nikwambie kamba, mtu akisha shiba huwa mwili unachoka na kupelekea kulala
(unalewa). Kwenye chakula kunamchanganyiko wa vitu vingi ambavyo vipo kwenye
chumvi ama sukari. Mfano ukinywa chai ni lazima usikie kulala tu! Kwani kuna sulpher ambayo inapelekea kulewa kwa akili na mwili.
Ndiyo maana ukishiba tu, unasikia kulala.
Mara nyingi
mimi napenda kula mchana vizuri, halafu usiku au jioni, huwa napenda kutumia
matunda na vitu laini visivyokuwa na mchanganyiko wowote. Huwa siwezi kusikia
uchovu kama vile ningekula chakula cha kawaida.
- MARA NYINGINE OMBA NA RAFKI YAKO. (Mhubiri 4:9-10)
Biblia inasema ”Ni heri wawili kuliko mmoja”. Kuna
faida ya kuomba pamoja na rafiki yako. Kwanza, mnapokuwa wawili au watatu,
inaleta hamasa na ari ya kuomba zaidi. Si rahisi kujisikia mvivu unapokuwa na
waombaji wenzako. Pili; nguvu ya kiroho inaongezeka. Neno linasema, mwombaji
mmoja anafukuza adui elfu moja, bali wakiwa wawili, wanafukuza elfu kumi, (siyo
elfu mbili! Ni elfu kumi!, (Kumb 32:30). Hiyo ni kanuni ya mbinguni/Ki-Mungu.
Kadri mnavyoongezeka, ndivyo na nguvu ya Mungu inaongezeka.
Hivyo,
wakati mwingine omba na rafiki yako unayemwamini, unayeweza kumshirikisha mambo
yako ya binafsi. Mashujaa wengi wa imani, walikuwa na marafiki zao wa kiroho.
Mfano:- Mathayo 17:1-9.
§
Musa – alikuwa na Joshua, Haruni na
Huri.
§
Eliya – alikuwa na Elisha
§
Elisha – akaja akawa na Gehazi
§
Daniel – alikuwa na Shadrack, Meshack
na Abednego.
§
Yesu – alikuwa na Petro, Yakobo na
Yohana.
§
Paulo – alikuwa na Barnaba, Timotheo na
Tito.
Kama
huna rafiki wa karibu wa kuomba naye, usikurupuke kujichagulia. Tulia umwombe
Mungu akupe mtu atakayekuwa wa msaada kwako. Mtu mtakayefungamanishwa naye
katika roho, hata kama mko mbali mbali kijiografia, lakini katika roho mko na
umoja mzuri wa imani. (Mathayo 18:18-19)
- ITAMBUE MIKAO INAYOKUPA UHURU NA UPAKO UNAPOOMBA.
Kila mtu ana namna yake alivyozoea akiwa anaomba, lakini
kunamikao mingine ambayo ukajifunza/ukaiiga, inakupa upako, kutegemeana na
uelewa wa huo mkao unamaanisha nini mbele za Mungu. Katika kuomba kwa muda
mrefu, mkao uliouzoea utakusaidia kwenda mwendo mrfu. Yakupasa kujua nguvu yako
na udhaifu wako. Wakati wa kuomba, epuka mikao inayokuchosha haraka na tumia
miako inayokupa nguvu zaidi. Kwa mfano, ukiwa umechoka usipende kuomba kwa
kupiga magoti au kuegemea kitandani. Ni bora uombe ukiwa umesimama au unatembea
tembea, ili kuepusha usingizi na uchovu. Waliozoea maombi wengine huwa
wanabadilisha badilisha mikao ili isiwachoshe.
Mifano ya waombaji walioomba
kwa mikao tofauti na kwa sababu za Ki-Mungu.
- Mzee Ibrahimu: aliomba kwa kusimama, (Mwanzo 18:22)
- Kusimama, maana yake kuutambua wajibu wako, kwenye eneo
lako, muda wako maalumu, na kile unachotakiwa kusimamia. (Habakuk 2:1)
- Daniel: aliomba kwa kupiga magoti. (Dan 6:10)
- Mtume Paulo: aliomba kwa kupiga magoti (Efeso 3:14)
- Bwana Yesu: aliomba kwa kupiga magoti. (Luka 22:41)
Nguvu iliyoko kwenye kupiga magoti. (Maombi ya Kujidhiri)
- Kupiga magoti huku unasali ni Ishara ya utii na
unyenyekevu mbele za Mungu. Mara nyingi wingu la Roho Mtakatifu na nguvu zake
huwa linamfunika mwombaji, inayopelekea ububujiko wa nguvu za Ki-Mungu ndani ya
mwombaji.
- Kupiga magoti ni Ishara ya uchaji wa Mungu ndani ya mtu
anayeomba.
- Unapopiga magoti na kuinama, mara nyingi unampa Roho
Mtakatifu kukusemesha jambo. Ufahamu wako na masikio ya kiroho huwa vinakuwa na
usikivu wa kiwango cha juu sana. (1Fal 18:42)
- Mungu alimuumba mwanadamu ili apate kushukuriwa na
kusifiwa na yeye (Mwanadamu). Unapopiga magoti unapeleka sifa na shukrani mbele
zake Mungu.
- Katika kupiga magoti, kunakumwabudu Mungu, kumheshimu
Mungu, Kumtukuza Mungu, kuwadhimisha Mungu na Kukubali kwamba Yeye ni Mungu.
Ndiyo maana unaweza ukapiga magoti na ukatulia, pasipo kuomba chochote, na
ukasikia nguvu fulani inashuka ndani yako. (Luk 22:41, Mdo 7:60, Mdo 9:40, Mdo
20:36)
Angalizo: Usipige magoti endapo mwili umechoka.
- Mfalme Suleiman: aliomba kwa kuinua mikono yake kuelekea juu mbinuni. (1Fal 8:22)
- Nabii Ezekiel: alisema mikono yetu tumwinulie Mungu Mbinguni (Maombolezo 4:41)
- Kuinua mikono juu ni Ishara ya utayari wa kufanya kile
unachoelekezwa.
- kuinua mikono juu ni ishara ya kujitoa mbele za Mungu.
- kuinua mikono juu ni Ishara ya utayari wa kupokea kile
unachokiomba, na kinafanyika sawa sawa na kiu iliyo ndani yako.
- Mikono kuinuliwa wakati wa maombi, ni Ishara ya
kuukunjua moyo wako mbele za Mungu na haja zako zote mbele zake.
NB: Usiombe kwa kupiga magoti endapo mwili na akili
vimechoka, utalala usingizi wala hutaweza kuomba.
- OMBA NA MUZIKI LAINI WA KUMWABUDU MUNGU.
Muziki wa kiroho, na wataratibu, unaweza kukutengenezea
mazingira mazuri sana ya kuomba kwa muda mrefu sana. Muziki wa kuabudu, unavuta
uwepo wa Mungu kwa namna ya kipekee sana. Neno linasema, ”waimbaji na wanamuziki
walipoimba na muziki ukapigwa, nao wakawa kama mtu mmoja, utukufu wa Mungu
ukashuka na kulijaza lile hekalu hata makuhani hawakuweza tena kuhudumu”
(2Nyak 5:12-14). Kule mbinguni, kila malaika wa sifa ana kinubi
(zeze/gitaa). Elisha hakuweza kutoa unabii mpaka mpiga kinubi alipopiga kwa
ustadi, ndipo mkono wa Bwana (Roho wa Mungu) alipokuja juu yake, naye akatabiri.
Nataka
uelewe, kwamba kunamuunganiko kati ya muziki wa kiroho na utukufu wa Mungu.
Hivyo ukiweza, unapokuwa kwenye mazingira ya kuomba unaweza weka cd au kanda
yenye nyimbo za taratibu na za kiroho. Siku hizi asilimmia kubwa simu zetu
zinauwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu, unaweza ukahifadhi nyimbo nyingi sana, hata
kwa kuchukua kwenye mtandao, na zikakusaidia kuvuta uwepo wa Mungu. Utajikuta
unaomba kwa muda mrefu sana bila hata kuchoka, na unatamani usiondoke kwenye
maombi.
- UJUE UNAOMBEA NINI
Biblia inasema ”Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi
mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea; naye
atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. (Mt 7:7-8). Huwezi kuomba
kama hujui unachokiomba (uhitaji wako), huwezi kutafuta kitu usichokijua. Wapo
watu wengi sana huwa wanaingia kila siku kwenye maombi, lakini hawana ajenda
maalumu wanazoziombea. Biblia inasema ”Haya, leteni maneno yenu, asema BWANA;
toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo.....Unikumbushe, na tuhojiane;
eleza mambo yako, upate kupewa haki yako” (Isa 41:21; 43:26).
Mimi huwa ninaziandika
ajenda za kuombea, kwenye karatasi dogo tu, na huwa nalishika mkononi, ndipo
ninaanza kuombea hizo ajenda, na ninauhakika ninapokuwa naziandika, huwa nakuwa
naziandika ndani ya moyo wangu na moyo wa Mungu, maana Yeye najua ndiye
aliyeniongoza mpaka nikaziandika. Nikisha anza kuomba naweza nikafunikwa na
nguvu kwa namna ya ajabu sana, maana nakuwa niko na mzigo na huku nikinena kwa
lugha maana najua Roho Mtakatifu ndiye anayeniombea
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni