Mungu aliumba kwanza vitu na
wanyama kabla ya mwanadamu, mwanadmu akaumbwa siku ya sita ambayo ilikuwa ni ya
mwisho ya uumbaji wake. Mwanadamu aliumbwa siku ya mwisho, bada ya Mungu kuona
hana haja ya yeye kukaa hapa duniani na kusimamia kila kitu, akaona ni bora aumbe
mtu kwa mfano wake (Mwanzo 1:26), ili vitu vimtambue na vitiishwe chini
ya Adamu, Mungu aliamua “kumbarikia”. Neno “kumbarikia” anamaana ni kuviweka
vile vitu kuwa chini yake na wengine wabarikiwe kutokana na yeye, pia ni ili
Adamu awe na sauti kwa kila kiumbe na kila kitu, na kisiwepo cha kumdhuru.
Nataka uone jambo fulani kwenye Mwanzo
1:28 inasema:
“Mungu
akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na
kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe
chenye uhai kiendacho juu ya nchi”
Angalia mistari mingine kwenye Mwanzo 9:1
Inasema “Mungu
akambariki Nuhu na wanawe, akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi”
Kusudi lake Mungu ni ili
mwanadamu azaliane na kumiliki, kila kitu kiwe chini yake kwa kila kizazi na
kizazi. Lakini baada ya dhambi kutokea, tunaona hali ya kutiisha imeondolewa
kwa mwanadamu, na kutokea hali ngumu. Na hiyo hali imekuwa ngumu kwa kila
mwanadamu, siyo Adamu tu! Na ndiyo maana Kaini na Habili waliamua kuutafuta uso
wa Bwana, kwa kutoa sadaka ilimradi waweze kupunguziwa magumu waliyokuwa
wanakumbana nayo kutokana na maisha yalivyokuwa chanzo ikiwa ni baba yao (Adamu).
Adamu ilimgharimu sana baada ya kufa kwa
Habili ambaye alipata kibali machoni pa Mungu, ilimgharimu kwa kumtafuta Mungu
apate kumleta mwana mwingine, atakaye fanana naye (Adamu) ili Mungu aendeleze
kusudi ndani ya mwana aliyesafi.
“Adamu akaishi
miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita
jina lake Sethi” (Mwanzo 5:3)
Mungu alikuwa anahitaji aanze
kujitukuza kwa watu kupitia Sethi (Mwanzo 4:26b) “…Hapo ndipo watu
walianza kuliitia jina la BWANA” ni baada ya Sethi kuzaliwa. Swali
langu, kwa nini Adamu asitubu ili Mungu amtumie yeye watu kuliitia jina la
BWANA?
Nilisikilize itakusaidia sana. Mungu
anamweshimu sana mwana, kwani anakuwa anaachilia kusudi fulani ndani ya wana,
na ndiyo maana hujaona Adamu baada ya kutenda dhambi akitoa sadaka wala akiutafuta
uso wa BWANA, bali Kaini na Habili ndiyo walioingia kwenye kumtafuta Mungu.
Nyie wazazi mnapokuwa mnaishi na familia zenu, kumbuka unatakiwa kuishi kwa
kumtengenezea mtoto siku zake za mbele (Vision) yaani kila unalolifanya
usifanye kwa ajili yako, bali fanya kwa ajili ya watoto wanaokuja kusudi jina
la BWANA lizidi kutukuzwa.
".......Maana sivitafuti vitu vyenu, bali nawatafuta ninyi (wazazi), maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa watoto" (2Kor 12:14b)
".......Maana sivitafuti vitu vyenu, bali nawatafuta ninyi (wazazi), maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa watoto" (2Kor 12:14b)
Kama Mungu amekupa uzao na kukupa ahadi
za kwenda kuitiisha nchi, inamaana uingie gharama za kumtafuta na kumlea mtoto
aliye kama Sethi, kusudi jina la BWANA lianze/liendelee kuitiwa, watu wamjue
Mungu kupitia huyo mwana, bali usitengeneze kizazi cha Kaini. Maandiko yanasema
“Kaini akaondoka mbele ya uso wa BWANA…” (Mwanzo 4:16a). Kaini alizaa mpaka vizazi
saba na vyote havikumjua Mungu kwa sababu aliondolewa mbele za Bwana, na
haikuwa shida ya watoto wake bali ya baba yao (Kaini) kwani hakuingia gharama
ya kutengeneza na kutubu baada ya kumuua ndugu yake (Habili) bali alibishana na
Mungu kwa lile alilotenda! Angejua Kaini, angewataarifu watoto wake habari za
Mungu pamoja na dhambi yake, pengine wangetubu na wangeanza kumtafuta Mungu.
“Waarifuni
watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, na watoto wao
wakakiambie kizazi kingine”
(Yoeli 1:3)
Panda mbegu ya neno la Mungu
ndani ya watoto, ili kizazi na kizazi kipate kuwa na hofu ya Mungu, usitake
kuwa kama Kaini, aliyekianzisha kizazi ambacho hakikumjua Mungu.
Si wazazi wengi sana
wanaotambua kusudi la Mungu kuwapatia watoto (uzazi), lakini nataka nikupe
angalau sababu kidogo:
Itaendelea..................................Barikiwa
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni