Nilipokuwa nasoma Injili ya Mathayo
sura ya kwanza, inaeleza uzao wa Bwana wetu Yesu Kristo tangu Adamu mpaka
Yeye. Nikaona kwamba Yesu tunamwita Mwana wa Daudi lakini Daudi hakuwa upande
wa Mariamu ambaye alimzaa Yesu, ila Yusufu aliyekuwa mchumba wa Mariamu ndiye
aliyekuwa ni wa uzao wa Daudi, na ukiangalia Yusufu naweza kusema hakuusika kwa
njia ya damu kwenye uzao wa Yesu bali Mariamu ambaye alikuwa ni mchumba wa
Yusufu maana ndyiye aliye tungiwa mimba ya Yesu. Swali langu kulikuwa na nini
mpaka Yesu akaitwa mwana wa Daudi? Yusufu na Mariamu walikuwa ni wachumba
lakini hawakuwahi kushiriki tendo la ndoa mpaka Yesu anazaliwa, na alizaliwa
kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, sasa ataitwaje Mwana wa Daudi ambaye alikuwa ni
upande wa Yusufu?
Nisikilize! Mbele za Mungu hakuna
mchumba bali kuna mke! Kipindi kile Yesu anazaliwa, walikuwepo waliokuwa bikra
wengisana na siyo Mariamu peke yake, lakini kwa heshima ya Yusufu na ahadi
aliyoitoa Mungu kwamba Bwana Yesu atazaliwa kwenye ukoo wa Daudi, ndiyo maana
ikatokea kwa Mariamu ambaye alikuwa ni mchumba (mke) wa Yusufu. Na ndiyo maana
nataka uelewe ya kuwa unapokuwa kwenye uchumba, unakuwa tayari upo kwenye
mtihani wa kuingia rasmi kwenye uthibitisho wa Mungu, na ndiyo maana unapewa
cheti unapofunga tu ndoa kanisani kuthibitisha kwamba umeweza mitihani ya
kwenye uchumba. Na mtihani wenyewe ni namna gani unaweza ukaudhibiti mwili wako
wakati wa uchumba, ni pale unapotaka kuingilia kusudi la Mungu kwa kutaka
kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa.
i)
Mtafute sana
Mungu.
Mungu anapokuonesha mke/mume
anamaana uendelee kumwobea na kuutafuta uso wa Bwana. Mungu anapoona moyo wako
wote na upendo wako wote umehamia kwa huyo mchumba, Mungu anachofanya
anawatenganisha kwa kuwafarakanisha, hicho kitu nimekiona kabisa, kuna rafiki
yangu alikuwa vizuri sana kiroho alipokuwa akitafuta mke na kweli Mungu
akamwonesha na akathibitisha, sasa shida iliyokuwepo ni yule ndugu alipunguza
muda wa maombi, akapunguza kusoma neno, hivyo muda wote alikuwa akitumia Simu
kuongea na huyo mchumba, mara baada ya miezi miwili akawa ameshuka kiroho
kabisa. Mungu alichokifanya akawagombanisha kwa sababu ndogo sana
iliyopelekea yule msichana kufikia kusema “sikutaki kabisa” na alidai amepata
mtu mwingine, sasa ilimbidi yule kijana aanze tena kuutafuta uso wa Mungu tena,
na ilimgharimu sana hadi Mungu kuanza kusema
naye kama hapo awali.
Unapoutafuta uso wa Mungu, Mungu huwa
anaachilia hekima namna gani ya kuweza kuishi maisha ya ndoa, unaweza ukawa na
umri mkubwa sana lakini huna hekima ya kuweza kulea ndoa na ndiyo maana
utashangaa mtu anachumbiwa/anachumbia mara ghafla mambo yanaharibika, ujue
Mungu hataki kuaibisha ndoa za Kikristo kwani wengi wakiingia ndani ya ndoa
wanashindwa kuwa na hekima namna gani ya kulea hizo ndoa, huwa inakuwa kila
siku ni kesi kwa wachungaji mara wazee wa kanisa, kitu ambacho siyo kizuri,
hivyo unapopata mwenzi endelea kutafuta mapenzi ya Mungu juu ya hiyo ndoa
unayoiendea.
Tegemea kupata watoto unapoingia kwenye
ndoa, kama huna mpango wa kuzaa watoto basi hilo mi sijui, lakini ninalojua moja ya
madhumuni ya Mungu kufanya ndoa ni ili watu wakazae na kuongezeka (Mwanzo
1:28) au la uwe na matatizo yako binafsi. Wasichana wengi hasa wa kizazi
hiki huwa wanashindwa kuwalea watoto kimaadili, pia hata uvivu wa kuwahudumia
vile ipasavyo. Kuna msichana mmoja nikawa namuuliza, hivi wewe katika maisha
yako ungependa kuzaa watoto wangapi na kwa muda gani? Akasema kwanza nikiolewa
tu nitakaa miaka miwili bila kuwa na mtoto halafu ndipo nitaamua kuzaa,
nikamuuliza kwanini? Akasema watoto ni wasumbufu sana ! Huyu alionesha uvivu wa hali ya juu
sana na hana ujasiri wa kuweza kukabiliana na kila jukumu lililoko mbele yake,
ingia kwenye kuutafuta uso wa Bwana ili akupe hekima na ujasiri namna ya kubeba
majukumu ya ndoa.
ii)
Vunja ukaribu.
Usipende kuwa karibu sana na
mchuma wako, kwa wale ambao wapo jirani au wanasali kanisa moja, na kwa wale
walio mbali, siku hizi kuna Simu hivyo huwa wanaongea sana na kwa muda mrefu
kitu ambacho siyo kizuri, mnapokuwa mmekuwa karibu sana kwa namna hiyo huwa
Shetani anapata nafasi sana na lazima siku moja mtagombana tu! Tena kwa sababu
ya Simu au meseji ama sababu ndogo tu. Kulikuwepo na rafiki yangu ambaye kila
siku alikuwa anaongea na mchumba wake hata mara ishirini, kwani ilikuwa kila
analofanya huwa anamwambia, sasa kijana wa kiume hakupokea simu mara mbili,
yaani kilichofuata ni matusi na kumwambia umenichoka najua unawengine, sasa kwa
taaarifa yako hata mimi ninao huku wengi tu! Huyo binti alikuwa akimwambia
kijana, basi ikawa ndiyo mwisho wa mahusiano yao .
Hawa wanaokuwa karibu, mara nyingi sana
wanaingia na tamaa ya kufanya uzinzi, nakumbuka kijana fulani mkoa fulani
sitaki kutaja, alienda kwa mchungaji na kumwambia uniongoze tena sala ya toba
upya kwani nimezini, akasema alikwenda kwa mchumba wake wa kike akaingia mpaka
chumbani na akajilaza kitandani, na baadaye alipokuja binti, yule kijana
akaingiliwa na tamaa ya kuzini na kwa kumlazimisha yule msichana mpaka wakaweza
kuzini, cha kusikitisha, wanasali pamoja na ni wapendwa ambao watu wanawaona
wamesimama, na siku hiyohiyo msichana mimba iliingia. Unisikilize msichana,
haijalishi unataka uimarishe uchumba au upendo kwa namna gani, maana wengine
wanasema nisipomridhisha leo hawazi kunioa, wewe mwambie kama
Mariamu kwamba; Yusufu ukiamua kuniacha kwa siri kwa ajili ya Yesu niliyembeba
we niache, lasivyo ukubari kunioa na huyu Yesu niliye naye, usikubali kumchafua
yesu ndani yako.
Usikubari mzoeane sana, kwani
mtakapoingia kwenye ndoa mtajikuta ni watu kama wa kawaida tu (dada na kaka),
kiasi kwamba unatakiwa unapoingia kwenye ndoa kila mmoja anamwona mwenzake kuwa
mpya, mkizoeanana sana inafikia baadaye mnakinaiana na mpaka inafikia
kudharauliana hatimaye kila mmoja ataanza kuona mwenzake kama siyo chaguo lake
mwishowe kuvunjika kwa uchumba.
Mnaweza mkawa mnafanya kazi ofisi moja,
itawabidi mtengeneze nidhamu ya kipekee sana .
Nakumbuka tulikuwa nchi fulani sitaki kuitaja, tulikuwa kikazi na tulikuwa watu
wengi kidogo kwani tulienda kwa ajili ya semina, sasa katikati yetu kuna watu
walikuwa ni wachumba, cha ajabu ni pale wakati wa kwenda kulala, na kwa sababu
tulifikia Hotelini ilikuwa ni lazima tulale tofauti tofauti, sasa wao ilikuwa
ni kitu kigumu sana ndipo wakataka kutumia nafasi ile kufanya ufuska wao,
ikapelekea kila mmoja wetu akagundua ule mchezo waliokuwa wanataka kufanya,
mpaka wakakalishwa kikao na wasimamizi. Sasa ni aibu sana
kwa picha kama hii na inaonekana nidhamu
hawana.
MWENDELEZO WA SOMO
Ukisoma Mathayo 1:18-25, Utapata habari za Yusufu na Mariamu mama yake na Yesu, utagundua kwamba baada ya Yusufu kumwona Mariam anaujazito wa Yesu na hawajawahi kukutana kimwili, lile jambo lilimfanya Yusufu aanze kumwacha kwa siri Mariamu. lakini kile kitendo cha Yusufu kutaka kumwacha Mariam kilimpa Mungu nafasi ya kumthibitishia Yusufu uchumba wao, na Mungu alisema usimwache mkeo! na Yusufu akajirudi, lakini fikiria Yusufu angeamua kukaa tu naye kwa sababu ya kupenda lakini akiwa na kinyongo ndani yake kwamba Mariam amepata mimba nje ya ndoa ingekuwaje! Mungu aliamua kusema kwa sababu Yusufu alijaribu kujitenga na Mariamu. hivyo unapovunja ukaribu na mchumba wako inampa nafasi Mungu kusema na kufanya jambo katika mahusiano yenu, na kama siyo wa kwako itajulikana hapo. wengi wameoana na siyo makusudi ya Mungu bali ni kwasababu walijiambatanisha wao kwanza na Mungu akawa hana nafasi ya kusema nao.
MWENDELEZO WA SOMO
Ukisoma Mathayo 1:18-25, Utapata habari za Yusufu na Mariamu mama yake na Yesu, utagundua kwamba baada ya Yusufu kumwona Mariam anaujazito wa Yesu na hawajawahi kukutana kimwili, lile jambo lilimfanya Yusufu aanze kumwacha kwa siri Mariamu. lakini kile kitendo cha Yusufu kutaka kumwacha Mariam kilimpa Mungu nafasi ya kumthibitishia Yusufu uchumba wao, na Mungu alisema usimwache mkeo! na Yusufu akajirudi, lakini fikiria Yusufu angeamua kukaa tu naye kwa sababu ya kupenda lakini akiwa na kinyongo ndani yake kwamba Mariam amepata mimba nje ya ndoa ingekuwaje! Mungu aliamua kusema kwa sababu Yusufu alijaribu kujitenga na Mariamu. hivyo unapovunja ukaribu na mchumba wako inampa nafasi Mungu kusema na kufanya jambo katika mahusiano yenu, na kama siyo wa kwako itajulikana hapo. wengi wameoana na siyo makusudi ya Mungu bali ni kwasababu walijiambatanisha wao kwanza na Mungu akawa hana nafasi ya kusema nao.
iii)
Ukweli na uwazi
Wakati wa uchumba ndiyo kipindi
ambacho utatakiwa kumchunguza na kumfahamu mwenzi wako, wapi ni mdhaifu na wapi
yupo imara, kusudi ujipange namna gani ya kumsaidia pindi utakapoingia kwenye
ndoa, na endapo mwenzako hatakubaliana na udhaifu utakaokuwa nao, basi huyo
Mungu hakukusudia mje kuishi pamoja. Kijana mmoja tulikuwa wote chuoni, alikuwa
na mchumba wake na wote wameokoka vizuri sana ,
sasa ghafla akaja akaniambia “nataka nikwambie kwamba fulani siyo mchumba wangu
tena!” Mi nikashangaa, kwani hawa watu tayari hata nyumbani kwao wanatambuana,
aliponipa sababu akasema mimi sikujua kwamba mtu mzima kama
yule anaweza akawa anakojoa kitandani, na juzi ndiyo nimejua napo hajaniambia
yeye! Nikashangaa sana kiasi kwamba nikaona
kwamba Mungu hakupanga hawa wawili waje kuishi pamoja, kwani hiyo ni sababu
ndogo sana , na
inamana angekuwa ni yeye je!
Kuna mambo mengine ambayo ni muhimu
wakati wa uchumba kuweza kuambiana ukweli na mengine siyo uyafunue, haswa ya
kifamilia. Ndoa nyingi zimekuja kusumbua kwa sababu baada ya kuingia kwenye
ndoa ndipo unakuja kutambua kwamba kumbe mmojawapo anamtoto tayari huko nje, na
hakukwambia mpaka mmekuja kufunga ndoa. Huwa yanatokea sana siku hizi, na kwa sababu vijana wengi
wanaonana mjini au chuoni, ghafla wanapendana na wanafikia mpaka ndoa hata bila
kujua historia ya mwenzake huko walikotoka. Fikiria ndiyo mnaenda kusalimia na
kutambulishana kwa wazazi kijijini baada ya kuoana, sasa ndiyo unakutana na
familia ya huyo mwanamke/mwanaume si utazimia!
iv)
Usitumie udhaifu wa mwenzio
Uchumba siyo kuumizana, msiingie
kwenye ndoa mkiwa na vidonda vilivyotokana na kipindi cha uchumba. Hizi hali
huwa zinatokea sana , kijana wa kiume anapoufunua
upendo wake kwa msichana, na pindi msichana anapotambua kwamba anapendwa sana na mchumba wake, huwa
kinachotokea yule msichana anadiriki kumwendesha mwenzake kwa kila hali,
analosema anataka ndivyo iwe hivyo. Muda mwingine anajaribu mpaka kumwmbia ya
kwamba mi ntakuacha endapo wakizozana kidogo, sasa vitu kama
hivyo baadaye vinaleta athari kwenye ndoa. Kuna ndoa niliwahi kuiona mkoa
fulani yaani mwanamume anapigwa na mke wake, kisa yule mwanamke alikuwa ni
mzuri sana wa sura, sasa mume wake alikuwa
amempenda sana
mke wake hivyo anaona bora apigwe tu lakini mke aimwache. Ndoa nyingine niliona
mwanamke alikuwa na hela kuliko mwanamume, sasa inapofikia wakati wa kupika
chakula alikuwa anaambiwa mwanamume akapike.
Mshukuru Mungu pale mwenzio anaonesha
upendo wa dhati kwako, nawe jitahidi uoneshe upendo kwake, kunawengine
wanatamani sana kusikia hata neno “I love
you” kwao ni adimu sana . Sasa wewe unaambiwa kila dakika hayo
maneno na yanakupa kiburi cha kumnyanyasa mwenzako, muda mwingine unaweza ukawa
unajaribu kama kumpima, lakini kumbe nawe
unampenda kweli, sasa siku akaamua kukata tama na mawasiliano ndipo
utakapotambua thamani yake.
“Mwanamke
akamwambia, wawezaje kusema nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami?
Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi” (Waamuzi
16:15)
Ni habari za Samsoni na Delila,
na maneno hayo alikuwa akiyasema Delila akimwambia Samsoni pale alipokuwa
anahitaji kujua asili ya nguvu zake, hivyo Delila alijua hana namna yoyote ile
ya kumbana Samsoni ili aseme asili ya nguvu zake, lasivyo amwambie suala la
upendo kwamba akiendelea kumdanganya basi Delila ataachana na Samsoni, na kwa
sababu Samsoni alimpenda sana Delila hivyo ilimlazimu Samsoni kumwambia siri ya
nguvu zake. Ndivyo ilivyo siku hizi, kijana akimpenda sana
msichana huwa anabanwa sana
mpaka hela zote zinakwenda kwa msichana hata kabla ya ndoa.
Wasichana wengine huwa wanapokuwa na
marafiki zao, huwa wanatabia ya kulingishiana wachumba zao, kwamba yupi
anapendwa sana
na mchumba wake. Wanafikia mpaka kushindana kwamba “mimi wa kwangu ana hela,
nikimwomba hata saizi alfu hamsini anatuma” na wanaamua kuomba kwa huyo mchumba
wake, na asipotumiwa atakuwa ameaibisha na anajikuta anaingi kumchukia mchumba
wake kwa sababu ya kijinga. Na uelewe unapojitangazia kwa wenzako kwamba
unapendwa sana ,
sasa kwa taarifa yako kunawasichana wanamapepo ya kupenda wanaume wa wenzao,
utashangaa kesho mchumba wako yupo na rafiki yako.
INAENDELEA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni