MAMBO
SABA (7) MUHIMU YA KUTAFAKARI NA KUZINGATIA
WAKATI UNAFIKIRIA KUOA/KUOLEWA
Maisha ya ndoa
ni maisha ya kipindi cha mwisho kwa Mwanadamu kilicho na mitihani mingi sana,
kwani ni darasa tosha kwa wanandoa, na ndiyo maana katika uchumba unatakiwa
upitie misukusuko kwani ni mojawapo ya mitihani ili ufikie kupata cheti wakati
wa ndoa, na nikatafakari sana kwamba hapa duniani mwanadamu anapata cheti baada
ya kufaulu mitihani, lakini kwa ndoa nikashangaa mtu anapewa cheti kwanza ndipo
anapoingia kwenye mtihani wa maisha ya ndoa, sasa ni wewe kufaulu au kushindwa!
- Tambua unapoamua kuoa au kuolewa
unakuwa unaunganisha familia tatu tofauti na zenye mifumo tofauti ya kimaisha.
Familia ya
kwanza ni yenu nyie wawili yaani mke na mume, siyo rahisi kuweza kuishi kiraisi
na mtu amabaye amelelewa kwao na mazingira tofauti na ya kwako, malezi tafauti
kabisa, mawazo na mtazamo ni tafauti, mara ghafla mnaanza kuishi pamoja, na
mnatakiwa kuwekana wazi kwa kila jambo na kufanya maamuzi yasiyoweza kuwafanya
mgombane. Sasa katika nyie wawili mtegemee kujenga na kuzaa familia yenye
mtazamo na taswira tofauti na familia zenu mlikotoka. Na familia zinazokuja
hizi mbili ni upande wa mwanamke na upande wa mwanamume na kila familia ina
tabia zake.
Familia zingine badala ya baba kuwa kiongozi
wa nyumba, utakuta mama ndiye kiongozi wa nyumba, inamaana kila analosema mama
pale nyumbani ndilo linafwatwa, wala baba hawezi kuwa na maamuzi yoyote yale
juu ya uamuzi atakaoufanya mama, sasa chukulia ndiyo unaoa msichana kwenye hiyo
familia na ghafla anaanza kukuendesha na kuwa na sauti ndani ya nyumba kwa kila
kitu, na kwa sababu alikotoka kwenye familia yao ameona mama ndiye kiongozi na
mwenye sauti ya mwisho wa familia, na kwa sababu wewe mwanamume hayo mambo
kwako ni mageni basi lazima muingie kwenye ugomvi.
Umewahi kufikiri unaenda kuo/kuolewa
kwenye familia ambayo ni wachawi! Vijana wengi kwa sababu ya tamaa zao
wamejikuta wameishia kuoa/kuolewa na watu wachawi. Kuna kijana mmoja alikuwa ni
mtumishi mzuri sana na Mungu alikuwa anamtumia vizuri sana lakini ilipofika
kipindi cha kuoa akaaamua kuchagua binti fulani kanisani humohumo na huyo binti
alikuwa anaonekana yupo safi kiroho na alikuwa mzuri hata wa sura, lakini watu
walimshauri kwamba huyo binti hakufai na kwa huduma uliyonayo kwa kweli
itakufa. Yule mtumishi hakuweza kuelewa ushauri wa wale watu, alin’gan’gana
mpaka akamwoa yule binti na ilipofika kipindi wanapokuwa kwenye huduma vijijini
pamoja na watumishi wengine, yule mtumishi akawa anashindwa kutumika kama hapo
awali, mara Mungu akamfunulia mtumishi mwenzake, usiku akamwona yule mtumishi
anakabwa na mke wake mpaka anaelekea kufa, ndipo wakatambua kwamba yule binti
alikuwa siyo mzuri yaani alikuwa mchawi, basi mpaka sasa yule mtumishi anaishia
kuwa kama waumini wengine kanisani kwani huduma ndiyo imekwisha kabisa mpaka
sasa.
Familia zingine huwa ni wachafu sana , yaani siku ukaenda
nyumbani kwao ghafla bila taarifa, utashanga takataka mpaka mlangoni na mara
nyingine hata kupiga deki ndani ni shida tupu, sasa unajiuliza humu ndani
naingia nivue viatu au? Maana nikivua ni lazima nitachafuka na nisipovua
watasema hana adabu. Sasa umewahi kufikiria ndiyo mwanamke anakuja unamwoa
utashaagaa hata kitanda kutandika ni shida, nguo zinakaa mpaka sebuleni. na
wanaume, siku mke kasafiri utajua tu kwamba leo mke wa fulani kasafiri,
utashangaa kuona sebuleni pako ovyo, vitambaa ni balaa tupu utasema kunawatoto
walikuwa wanacheza na kama alikuwa anajipikia basi utavikuta vyombo vimejazana
na vinazungukwa na nzi, sufuria zina masizi mpaka ndani sasa sijui yaliingiaje
mi sijui! Ni aibu hiyo jamani!, sasa hali ikiwa kama
hivyo itapelekea magonjwa yasiyoeleweka. Badala ya kuona raha ya ndoa sasa
unaanza kuona karaha ya ndoa kisa hukufanya uchunguzi na kufikiria kabla
hujafanya maamuzi.
Watu wengine ni wavivu sana ,
maandiko yasema “asiyefanya kazi na asile”, kunafamilia zingine jamani
ni tabu tupu, ukiangalia wanapenda kuvaa vizuri sana
na kujipenda sana na kanisani wanaenda sana , lakini ukiuliza wapi
wanashamba la kulima watakwambia hamna. Kweli wengine wanaishi mjini mashamba
ambapo hamna lakini nina maana hata sehemu ya kujipatia riziki angalau kidogo,
wengine hata kujishughulisha na shughuli ndogondogo tu huwa hawawezi, hasa
vijana wa kiume utashanga kuanzia asubuhi mpka jioni anaangalia Vidio
(Television Vidio (TV)) na hapo anamchumba na anapanga kuoa, hata godoro hana
na bado anakaa kwa wazazi wake, yeye huwa anasubiri asubuhi ifike anywe chai
aliyopika mama au dada ndipo aende kijiweni na ikifika mchana atarudi kula
chakula cha mchana na kurudi tena kijiweni, hivyohivyo na jioni na kama ndiyo
siku ya ibada ndipo ataoga na kuomba sadaka kwa mzazi halafu aende kanisani.
Mhh Mungu atusaidie sana .
Familia zingine zinamazindiko sana , kwamba kila atakaye
mwoa huyu binti wa kwanza ni lazima afe, au wanamwapisha kwamba huyu binti
atakuwa anaishia kuwa mjane, pia hata upande wa mwanamume huwa mazindiko yapo,
kwamba huyu kijana kila akioa hatakuwa anapata watoto. Nilipigiwa simu siku
moja na binti, akaniambia nimwombee kwani alinenewa na shangazi yake ya kwamba
hatakuja kupata mume wala mafanikio yoyote katika maisha yake yote, na hapo
alipo alikuwa amewahi chumbiwa mara tatu na anaishia kuachwa pasipo na sababu,
na sasa anaishia tu kukaka kwa dada yake, usije kushangaa hata mwenyewe unajaribu
kupanga kuoa/kuolewa kumbe umefungwa lakini yote ni ushirikina wa kifamilia au
huo ukoo.
Pia kuna familia zingine au makabila
mengine huwa wanadai mtoto wa kwanza kuzaliwa ili atolewe kama
kafara, na usipoelewa hili litakugharimu pindi tu utakapokuja kumpoteza huyo
mtoto na ndipo utakapoelewa, na ndiyo maana tunasema kijana kaa vizuri na Mungu
naye atakupa macho ya rohoni utaona wapi panafaa kuoa/kuolewa. Kumbuka pia
magonjwa mengine ya kurithi huwa yanafwatilia watoto wa kwanza kama vile kuugua kichaa, kifafa, kifua kikuu, UKIMWI n.k
na hizo zinakuwa ni roho tu zinazofuatilia familia. Kumbuka unapounganisha
mambo yote ya familia ya upande huu na upande mwingine unategemea utapata nini
hapo?
- Unapoamua kuoa/kuolewa utambue
unaenda kuwajibika zaidi
Kumbuka ya
kwamba unapoamua kuoa/kuolewa unaenda kuanza maisha ya kipekee kwani hiyo ndiyo
ngazi ya maisha yako ya mwisho mpaka kufa kwako, kumbuka siku utaitwa baba/mama
mpaka utakuja itwa bibi/babu, kama Mungu
atakujalia maisha marefu, hivyo kumbuka utakuwa umekusanya ndugu wa pande mbili
zote, sasa usije sema mi naweza nikamlea mke wangu tu! Hapana, kumbuka kuna
ndugu wa upande wa mke/mume wako watahitaji msaada je utaweza kumudu? Na
maandiko yanasema;
“Lakini
mtu yeyote asiyewatunza walio wake, yaani wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana
Imani tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini” (1Timotheo 5:8)
Ni aibu na ni
dhambi, pale unaposhindwa kuwahudumia ndugu zako wa nyumbani mwako, kumbuka
kunamaradhi, kuna misiba, kuna wengine wanasoma kama
mdogo mtu au kaka mtu hao watahitaji matumizi ya shule au ada, kuna mambo
ambayo ulipokuwa peke yako uliona ni rahisi kufanya lakini pindi unapokuwa na
ndoa unatakiwa kuwajibika zaidi.
Mara nyingine kwa kijana wa kiume unaoa
msichana ambaye ni wa kwanza kwao au ni tegemeo kwenye familia yao , na pindi unapoamua
kumwoa inamaana tegemeo lote linakuwa ni wewe, sasa sikwambii usimwoe! Hapana,
baali hakikisha umejipanga vizuri kukabiliana na majukumu aliyokuwa nayo kwao
kwani huwezi kuwatupa ndugu wa upande wake, na siku nyingine watapenda kuja
kukutembelea kwako, na wengine watapenda kulala kama ni mbali kidogo, sasa
itategemea umejenga nyumba au umepanga nyumba ya namna gani, nasema hivi kwani
nimeona pindi tu wanandoa wanapoingia wakiwa hawana hata muda mrefu huwa inaanza
misuguano na ukifwatilia utakuta ni ndugu wanajaa nyumbani. Sasa jiandae
unaeingia kwenye ndoa kubeba ugeni na kuwajibika kwa hali na maali.
Kumbuka kunakuwajibika kimawazo pia,
muda mwingine kunakuwepo na vikao mbalimbali vya familia ya upande wa mwenzi
wako, nawe kama mwanafamilia unatakiwa kuwa na
upeo wa kuweza kuchangia hoja na mawazo ya kimsingi, utashangaa shemeji mtu
kwenye kikao anakuja ananuka pombe na anayoyafanya pale kwenye kikao mwenyewe
mwenzi wake utatamani uzimie. Sasa kama yeye mwenyewe anashindwa kujilekebisha
ataweza kweli kumpa mtu mawazo ya kumjenga? Na ndiyo hao wanafika kipindi
wanatembea na wafanya kazi wao wa ndani na inayopelekea mpaka ndoa kuyumba.
Hasa kwa mabinti nataka mnisikilize, ni
aibu sana binti
unaeingia kwenye ndoa halafu hujui kupika, unapika wali jinsi unavyoukologa
loh! Utazani unakologa uji, na ukipika ugali unaekula utatakiwa uwe na maji ya
moto pembeni kwani lazima ukutane na mabonge ya unga katikati ya ugali, sasa ni
aibu na ndiyo maana wanaume wanaamua kula huko nje ndipo wanarudi nyumbani. Pia
wanaume nanyi mnashangaza sana wengine hata
kusonga ugali ni shida sana ,
na pindi mke anumwa wewe unaamua kununua chipsi, sasa sijui mtakulahizo chipsi
mpaka lini, siku umeingia jikoni unaipua ugali mbichi kabisa. Nakumbuka
nilitembelewa na rafiki yangu mmoja na mimi nilikuwa sishindi nyumbani, na pale
nyumbani kuna kila kitu cha kuweza kupika, siku nimetoka kazini narudi nyumbani
nikakuta hajapika kitu, nilipomuuliza mbona hujapika? Na umekula nini? Akasema
nilinunua chipsi, nami nikajua aliamu tu kununua chipsi pengine kwa sababu ya
uchovu, sasa kesho yake nikamwabia twende sokoni ukaje na mboga kwani mimi
sitarudi! Tulipofika sokoni nikanunu mboga na nilipomwambia aendelee kupika,
akasema utakuja kupika mwenyewe kwani mimi sijui kupika! hah! Yaani nilishikwa
na butwaa, na nikweli kabisa alikuwa hajui na alikuwa kijana amemaliza chuo
kikuu.
Sasa unielewe kwamba unapooa unaenda
kuwa na mipaka, kwamba ni lazima ukawajibike tu na hiyo mipaka ni ya baadhi ya
mambo mengine kutokuyafanya, kama vile kurudi usiku nyumbani, kama ulikuwa
unakesha kuangalia mpira kwa jirani yako sasa itabidi hiyo tabia ife , kwani siku utarudi
utakuta mwana si wako.
Kama bado hujaoa, weka mpangilio ni
lini unaoa kusudi upangilie mipango na namna gani utaweza kukabiriana na
majukumu, shida ipo sana
kwa vijana wakiona fulani kaoa basi utashangaa naye huyu anakimbilia kuoa, we
unajua mwenzio alivyojipanga? Weka malengo ndani ya muda fulani utakuwa
umefanya mambo kadhaa ndipo uingine kwenye ndoa.
“Kwa
kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”
(Mhubiri 3:1)
Ujue kila
kipindi unachopitia kuna takiwa uchukue hatua za mabadiliko kutegemeana na
majira, na kama unajipanga kuoa baada ya miaka
miwili inamaana kunamambo utatakiwa kuyafanya hapa katikati ili kujiandaa
kukabiriana na majukumu ya ndoa. Pia kwa kadri tathmini utakavyokuwa unaiona ni
rahisi kuwa na taswira nzima ya ndoa yako na kujua watoto utakao kuja kuzaa.
Kunawengine wanaingia kwenye ndoa hata hawaelewi watazaa watoto wangapi na
wengine hata wakati wa uchumba huwa hawajadili kwamba waje wazae watoto
wangapi, sasa inapotokea mmeingia tayari kwenye ndoa na mwenzio anataka watoto
sita na wewe unataka wawili sasa sijui mtakata rufaa wapi, mimi sijui! Zaidi
mtakuwa mnaleta kuvutana kwenye suala la idadi ya watoto kila siku.
Unapoamu kuoa angalia kwanza wewe ni
tegemeo kwenye familia au lah! Unawadogo zako wanatakiwa kwenda shule na bado
hawajaenda au ndiyo wapo shule, elewa unapoingia kuoa kabla ya hao watoto
kuwawekea msingi mzuri ukitegemea kwamba ukioa utawasomesha, uwe na uhakika
kabisa watayumba kwani maamuzi yako ya kuwasomesha ukiwa kwenye ndoa ni lazima
umshirikishe mke wako, na siyo rahisi kukubali kila mwisho wa mwezi mshahara uende
nyumbani kusaidia ada ya wadogo zako, na mara nyingi familia zimekwama kielimu
na maendeleo mengine kwa sababu tu kaka aliyekuwa mwenye uwezo kaoa na baada ya
kuoa akasahau kusaidia wazazi na wadogo zake.
- Itaendelea.........................................
Masomo mengine: -
MAMBO
SABA (7) MUHIMU YA KUTAFAKARI NA KUZINGATIA
WAKATI UNAFIKIRIA KUOA/KUOLEWA
Maisha ya ndoa
ni maisha ya kipindi cha mwisho kwa Mwanadamu kilicho na mitihani mingi sana,
kwani ni darasa tosha kwa wanandoa, na ndiyo maana katika uchumba unatakiwa
upitie misukusuko kwani ni mojawapo ya mitihani ili ufikie kupata cheti wakati
wa ndoa, na nikatafakari sana kwamba hapa duniani mwanadamu anapata cheti baada
ya kufaulu mitihani, lakini kwa ndoa nikashangaa mtu anapewa cheti kwanza ndipo
anapoingia kwenye mtihani wa maisha ya ndoa, sasa ni wewe kufaulu au kushindwa!
- Tambua unapoamua kuoa au kuolewa
unakuwa unaunganisha familia tatu tofauti na zenye mifumo tofauti ya kimaisha.
Familia ya
kwanza ni yenu nyie wawili yaani mke na mume, siyo rahisi kuweza kuishi kiraisi
na mtu amabaye amelelewa kwao na mazingira tofauti na ya kwako, malezi tafauti
kabisa, mawazo na mtazamo ni tafauti, mara ghafla mnaanza kuishi pamoja, na
mnatakiwa kuwekana wazi kwa kila jambo na kufanya maamuzi yasiyoweza kuwafanya
mgombane. Sasa katika nyie wawili mtegemee kujenga na kuzaa familia yenye
mtazamo na taswira tofauti na familia zenu mlikotoka. Na familia zinazokuja
hizi mbili ni upande wa mwanamke na upande wa mwanamume na kila familia ina
tabia zake.
Familia zingine badala ya baba kuwa kiongozi
wa nyumba, utakuta mama ndiye kiongozi wa nyumba, inamaana kila analosema mama
pale nyumbani ndilo linafwatwa, wala baba hawezi kuwa na maamuzi yoyote yale
juu ya uamuzi atakaoufanya mama, sasa chukulia ndiyo unaoa msichana kwenye hiyo
familia na ghafla anaanza kukuendesha na kuwa na sauti ndani ya nyumba kwa kila
kitu, na kwa sababu alikotoka kwenye familia yao ameona mama ndiye kiongozi na
mwenye sauti ya mwisho wa familia, na kwa sababu wewe mwanamume hayo mambo
kwako ni mageni basi lazima muingie kwenye ugomvi.
Umewahi kufikiri unaenda kuo/kuolewa
kwenye familia ambayo ni wachawi! Vijana wengi kwa sababu ya tamaa zao
wamejikuta wameishia kuoa/kuolewa na watu wachawi. Kuna kijana mmoja alikuwa ni
mtumishi mzuri sana na Mungu alikuwa anamtumia vizuri sana lakini ilipofika
kipindi cha kuoa akaaamua kuchagua binti fulani kanisani humohumo na huyo binti
alikuwa anaonekana yupo safi kiroho na alikuwa mzuri hata wa sura, lakini watu
walimshauri kwamba huyo binti hakufai na kwa huduma uliyonayo kwa kweli
itakufa. Yule mtumishi hakuweza kuelewa ushauri wa wale watu, alin’gan’gana
mpaka akamwoa yule binti na ilipofika kipindi wanapokuwa kwenye huduma vijijini
pamoja na watumishi wengine, yule mtumishi akawa anashindwa kutumika kama hapo
awali, mara Mungu akamfunulia mtumishi mwenzake, usiku akamwona yule mtumishi
anakabwa na mke wake mpaka anaelekea kufa, ndipo wakatambua kwamba yule binti
alikuwa siyo mzuri yaani alikuwa mchawi, basi mpaka sasa yule mtumishi anaishia
kuwa kama waumini wengine kanisani kwani huduma ndiyo imekwisha kabisa mpaka
sasa.
Familia zingine huwa ni wachafu sana , yaani siku ukaenda
nyumbani kwao ghafla bila taarifa, utashanga takataka mpaka mlangoni na mara
nyingine hata kupiga deki ndani ni shida tupu, sasa unajiuliza humu ndani
naingia nivue viatu au? Maana nikivua ni lazima nitachafuka na nisipovua
watasema hana adabu. Sasa umewahi kufikiria ndiyo mwanamke anakuja unamwoa
utashaagaa hata kitanda kutandika ni shida, nguo zinakaa mpaka sebuleni. na
wanaume, siku mke kasafiri utajua tu kwamba leo mke wa fulani kasafiri,
utashangaa kuona sebuleni pako ovyo, vitambaa ni balaa tupu utasema kunawatoto
walikuwa wanacheza na kama alikuwa anajipikia basi utavikuta vyombo vimejazana
na vinazungukwa na nzi, sufuria zina masizi mpaka ndani sasa sijui yaliingiaje
mi sijui! Ni aibu hiyo jamani!, sasa hali ikiwa kama
hivyo itapelekea magonjwa yasiyoeleweka. Badala ya kuona raha ya ndoa sasa
unaanza kuona karaha ya ndoa kisa hukufanya uchunguzi na kufikiria kabla
hujafanya maamuzi.
Watu wengine ni wavivu sana ,
maandiko yasema “asiyefanya kazi na asile”, kunafamilia zingine jamani
ni tabu tupu, ukiangalia wanapenda kuvaa vizuri sana
na kujipenda sana na kanisani wanaenda sana , lakini ukiuliza wapi
wanashamba la kulima watakwambia hamna. Kweli wengine wanaishi mjini mashamba
ambapo hamna lakini nina maana hata sehemu ya kujipatia riziki angalau kidogo,
wengine hata kujishughulisha na shughuli ndogondogo tu huwa hawawezi, hasa
vijana wa kiume utashanga kuanzia asubuhi mpka jioni anaangalia Vidio
(Television Vidio (TV)) na hapo anamchumba na anapanga kuoa, hata godoro hana
na bado anakaa kwa wazazi wake, yeye huwa anasubiri asubuhi ifike anywe chai
aliyopika mama au dada ndipo aende kijiweni na ikifika mchana atarudi kula
chakula cha mchana na kurudi tena kijiweni, hivyohivyo na jioni na kama ndiyo
siku ya ibada ndipo ataoga na kuomba sadaka kwa mzazi halafu aende kanisani.
Mhh Mungu atusaidie sana .
Familia zingine zinamazindiko sana , kwamba kila atakaye
mwoa huyu binti wa kwanza ni lazima afe, au wanamwapisha kwamba huyu binti
atakuwa anaishia kuwa mjane, pia hata upande wa mwanamume huwa mazindiko yapo,
kwamba huyu kijana kila akioa hatakuwa anapata watoto. Nilipigiwa simu siku
moja na binti, akaniambia nimwombee kwani alinenewa na shangazi yake ya kwamba
hatakuja kupata mume wala mafanikio yoyote katika maisha yake yote, na hapo
alipo alikuwa amewahi chumbiwa mara tatu na anaishia kuachwa pasipo na sababu,
na sasa anaishia tu kukaka kwa dada yake, usije kushangaa hata mwenyewe unajaribu
kupanga kuoa/kuolewa kumbe umefungwa lakini yote ni ushirikina wa kifamilia au
huo ukoo.
Pia kuna familia zingine au makabila
mengine huwa wanadai mtoto wa kwanza kuzaliwa ili atolewe kama
kafara, na usipoelewa hili litakugharimu pindi tu utakapokuja kumpoteza huyo
mtoto na ndipo utakapoelewa, na ndiyo maana tunasema kijana kaa vizuri na Mungu
naye atakupa macho ya rohoni utaona wapi panafaa kuoa/kuolewa. Kumbuka pia
magonjwa mengine ya kurithi huwa yanafwatilia watoto wa kwanza kama vile kuugua kichaa, kifafa, kifua kikuu, UKIMWI n.k
na hizo zinakuwa ni roho tu zinazofuatilia familia. Kumbuka unapounganisha
mambo yote ya familia ya upande huu na upande mwingine unategemea utapata nini
hapo?
- Unapoamua kuoa/kuolewa utambue
unaenda kuwajibika zaidi
Kumbuka ya
kwamba unapoamua kuoa/kuolewa unaenda kuanza maisha ya kipekee kwani hiyo ndiyo
ngazi ya maisha yako ya mwisho mpaka kufa kwako, kumbuka siku utaitwa baba/mama
mpaka utakuja itwa bibi/babu, kama Mungu
atakujalia maisha marefu, hivyo kumbuka utakuwa umekusanya ndugu wa pande mbili
zote, sasa usije sema mi naweza nikamlea mke wangu tu! Hapana, kumbuka kuna
ndugu wa upande wa mke/mume wako watahitaji msaada je utaweza kumudu? Na
maandiko yanasema;
“Lakini
mtu yeyote asiyewatunza walio wake, yaani wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana
Imani tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini” (1Timotheo 5:8)
Ni aibu na ni
dhambi, pale unaposhindwa kuwahudumia ndugu zako wa nyumbani mwako, kumbuka
kunamaradhi, kuna misiba, kuna wengine wanasoma kama
mdogo mtu au kaka mtu hao watahitaji matumizi ya shule au ada, kuna mambo
ambayo ulipokuwa peke yako uliona ni rahisi kufanya lakini pindi unapokuwa na
ndoa unatakiwa kuwajibika zaidi.
Mara nyingine kwa kijana wa kiume unaoa
msichana ambaye ni wa kwanza kwao au ni tegemeo kwenye familia yao , na pindi unapoamua
kumwoa inamaana tegemeo lote linakuwa ni wewe, sasa sikwambii usimwoe! Hapana,
baali hakikisha umejipanga vizuri kukabiliana na majukumu aliyokuwa nayo kwao
kwani huwezi kuwatupa ndugu wa upande wake, na siku nyingine watapenda kuja
kukutembelea kwako, na wengine watapenda kulala kama ni mbali kidogo, sasa
itategemea umejenga nyumba au umepanga nyumba ya namna gani, nasema hivi kwani
nimeona pindi tu wanandoa wanapoingia wakiwa hawana hata muda mrefu huwa inaanza
misuguano na ukifwatilia utakuta ni ndugu wanajaa nyumbani. Sasa jiandae
unaeingia kwenye ndoa kubeba ugeni na kuwajibika kwa hali na maali.
Kumbuka kunakuwajibika kimawazo pia,
muda mwingine kunakuwepo na vikao mbalimbali vya familia ya upande wa mwenzi
wako, nawe kama mwanafamilia unatakiwa kuwa na
upeo wa kuweza kuchangia hoja na mawazo ya kimsingi, utashangaa shemeji mtu
kwenye kikao anakuja ananuka pombe na anayoyafanya pale kwenye kikao mwenyewe
mwenzi wake utatamani uzimie. Sasa kama yeye mwenyewe anashindwa kujilekebisha
ataweza kweli kumpa mtu mawazo ya kumjenga? Na ndiyo hao wanafika kipindi
wanatembea na wafanya kazi wao wa ndani na inayopelekea mpaka ndoa kuyumba.
Hasa kwa mabinti nataka mnisikilize, ni
aibu sana binti
unaeingia kwenye ndoa halafu hujui kupika, unapika wali jinsi unavyoukologa
loh! Utazani unakologa uji, na ukipika ugali unaekula utatakiwa uwe na maji ya
moto pembeni kwani lazima ukutane na mabonge ya unga katikati ya ugali, sasa ni
aibu na ndiyo maana wanaume wanaamua kula huko nje ndipo wanarudi nyumbani. Pia
wanaume nanyi mnashangaza sana wengine hata
kusonga ugali ni shida sana ,
na pindi mke anumwa wewe unaamua kununua chipsi, sasa sijui mtakulahizo chipsi
mpaka lini, siku umeingia jikoni unaipua ugali mbichi kabisa. Nakumbuka
nilitembelewa na rafiki yangu mmoja na mimi nilikuwa sishindi nyumbani, na pale
nyumbani kuna kila kitu cha kuweza kupika, siku nimetoka kazini narudi nyumbani
nikakuta hajapika kitu, nilipomuuliza mbona hujapika? Na umekula nini? Akasema
nilinunua chipsi, nami nikajua aliamu tu kununua chipsi pengine kwa sababu ya
uchovu, sasa kesho yake nikamwabia twende sokoni ukaje na mboga kwani mimi
sitarudi! Tulipofika sokoni nikanunu mboga na nilipomwambia aendelee kupika,
akasema utakuja kupika mwenyewe kwani mimi sijui kupika! hah! Yaani nilishikwa
na butwaa, na nikweli kabisa alikuwa hajui na alikuwa kijana amemaliza chuo
kikuu.
Sasa unielewe kwamba unapooa unaenda
kuwa na mipaka, kwamba ni lazima ukawajibike tu na hiyo mipaka ni ya baadhi ya
mambo mengine kutokuyafanya, kama vile kurudi usiku nyumbani, kama ulikuwa
unakesha kuangalia mpira kwa jirani yako sasa itabidi hiyo tabia ife , kwani siku utarudi
utakuta mwana si wako.
Kama bado hujaoa, weka mpangilio ni
lini unaoa kusudi upangilie mipango na namna gani utaweza kukabiriana na
majukumu, shida ipo sana
kwa vijana wakiona fulani kaoa basi utashangaa naye huyu anakimbilia kuoa, we
unajua mwenzio alivyojipanga? Weka malengo ndani ya muda fulani utakuwa
umefanya mambo kadhaa ndipo uingine kwenye ndoa.
“Kwa
kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”
(Mhubiri 3:1)
Ujue kila
kipindi unachopitia kuna takiwa uchukue hatua za mabadiliko kutegemeana na
majira, na kama unajipanga kuoa baada ya miaka
miwili inamaana kunamambo utatakiwa kuyafanya hapa katikati ili kujiandaa
kukabiriana na majukumu ya ndoa. Pia kwa kadri tathmini utakavyokuwa unaiona ni
rahisi kuwa na taswira nzima ya ndoa yako na kujua watoto utakao kuja kuzaa.
Kunawengine wanaingia kwenye ndoa hata hawaelewi watazaa watoto wangapi na
wengine hata wakati wa uchumba huwa hawajadili kwamba waje wazae watoto
wangapi, sasa inapotokea mmeingia tayari kwenye ndoa na mwenzio anataka watoto
sita na wewe unataka wawili sasa sijui mtakata rufaa wapi, mimi sijui! Zaidi
mtakuwa mnaleta kuvutana kwenye suala la idadi ya watoto kila siku.
Unapoamu kuoa angalia kwanza wewe ni
tegemeo kwenye familia au lah! Unawadogo zako wanatakiwa kwenda shule na bado
hawajaenda au ndiyo wapo shule, elewa unapoingia kuoa kabla ya hao watoto
kuwawekea msingi mzuri ukitegemea kwamba ukioa utawasomesha, uwe na uhakika
kabisa watayumba kwani maamuzi yako ya kuwasomesha ukiwa kwenye ndoa ni lazima
umshirikishe mke wako, na siyo rahisi kukubali kila mwisho wa mwezi mshahara uende
nyumbani kusaidia ada ya wadogo zako, na mara nyingi familia zimekwama kielimu
na maendeleo mengine kwa sababu tu kaka aliyekuwa mwenye uwezo kaoa na baada ya
kuoa akasahau kusaidia wazazi na wadogo zake.
1 Tambua madhara ya NGUVU YA AGANO KWENYE MAHUSIANO NA NAMNA YA KUTOKA ILI UFANIKIWE.
2 ZIFAHAMU CHANGAMOTO KATIKA MAHUSIANO YA UCHUMBA NA NAMNA YA KUZIKABILI.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni